• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Lushoto District Council
Lushoto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto

  • mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Muundo
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Utumishi na Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufatiliaji
        • Planning
      • Afya
        • Healthy
      • Fedha na Biashara
        • Finance
      • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
        • Elimu ya sekondari
      • Maji
        • water sector
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
        • Agriculture and Irrigation
      • Huduma za ufugaji
        • Huduma za ufugaji
      • Maliasili Ardhi na Mipango Mji
      • Maendeleo ya Jamii Wanawake Vijana Watoto na Wazee
        • Community development
      • Ujenzi na Zima Moto
        • Works and fire rescure
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
        • Internal Auditor unit
      • Teknolojia ya Habari na mawasiliano
        • Information communication and public Relation
      • Manunuzi na Ugavi
        • Manunuzi na Ugavi
      • Mazingira na Usafi
        • Environment and sanitation
      • Uchaguzi
        • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezajia
    • Vivutio vya Utalii
      • Tourist attraction investiment area
    • Kilimo
      • Agriculture Investment Areas
    • Mazao ya misitu
      • Forest products
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
      • Health services offered
    • Huduma za Elimu
      • Education services offered
    • Huduma za Kilimo
      • Agriculture services offered
    • livestock and fisheries services
      • livestock and fisheries services offered
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Uchumi Uongozi na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati za maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba mbalimbali
    • Ghala la Picha

Maendeleo ya Jamii Wanawake Vijana Watoto na Wazee

IDARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO.

Idara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ni mojawapo ya idara za Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto. Idara hii inaratibu utekelezaji wa shughuli mbalimbali zikiwemo uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, maendeleo ya watoto, usajili na uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, ushirikishwaji jamii, maendeleo ya jinsia na masuala mtambuka kama mazingira, rushwa, UKIMWI, Afya ya jamii, Bima ya Afya, jinsia na lishe.

   Maeneo ya kiutawala

Idara ya Maendeleo ya Jamii, jinsia, wazee na watoto ina jumla ya madawati matano ya utekelezaji ambayo ni Dawati la uwezeshaji wa wananchi kiuchumi na kupunguza umaskini (dawati linashughulika na kusimamia Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake, Vijana na Walemavu); Dawati la Ushirikishwaji jamii linaloratibu Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF; kuwezesha jamii kupanga na kutekeleza shughuli za maendeleo; kutambua fursa na vikwazo vya maendeleo ya jamii na namna ya kushirikisha jamii kushiriki kwenye shughuli za maendeleo; na kutoa elimu kwa jamii kuhusu miradi mikubwa ya kimkakati kama umeme na barabara inayotekelezwa na serik ali; Dawati la uratibu wa maendeleo ya jinsia; Dawati la uratibu wa maendeleo ya mtoto, Dawati la usajili na uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs); na Dawati la uratibu wa masuala mtambuka (Utunzaji wa Mazingira, Jinsia, Mapambano dhidi ya Rushwa, Mapambano dhidi ya UKIMWI, Afya ya Jamii, Bima ya Afya na Lishe).

 

    Malengo ya Idara

Kuwezesha jamii boresha ustawi wa hali ya maisha, kupata haki na kupata huduma bora za kijamii na kiuchumi kwa kushirikishwa na kushiriki  katika kupanga, kuamua, kutekeleza, kusimamia na kutathimi shughuli za maendeleo.

 

  Majukumu ya Idara

Idara ya Maendeleo ya Jamii, jinsia, wazee na watoto inatekeleza majukumu yafuatayo:

  • Kushirikisha Jamii katika kuainisha fursa na changamoto zinazoikabili ili kulijiletea Maendeleo.
  • Kuelimisha jamii kupanga na kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kuzingatia rasilimali zilizopo.
  • Kuelimisha Jamii kuondokana na Fikra, Imani, Mila, Desturi na Tamaduni zinazokinzana na Maendeleo.
  • Kushirikisha Jamii katika kuiunganisha na kuwezesha makundi maalum katika kubaini fursa na mchakato wa maendeleo ili kuinua ustawi wa maisha ya wanajamii.
  • Kuratibu utekelezaji na uzingatiaji wa masuala ya jinsia katika programu na mipango ya maendeleo katika sekta mbalimbali.
  • Kujenga uwezo kwa viongozi wa Halmashauri za vijiji/mitaa na serikali za mitaa juu ya dhana ya utawala bora.
  • Kuwezesha jamii kutumia fursa ya sera za kisekta na mikakati yake katika kujiletea maendeleo.
  • Kuwezesha wananchi kunufaika na fursa za kiuchumi.
  • Kuwezesha jamii kutekeleza haki na malezi ya mtoto.
  • Kuwezesha usajili, kuratibu na ufuatiliaji wa mashirika yasiyo ya kiserikali.
  • Kuwezesha jamii kutambua, kuanisha na kuzuia migogoro inayoathiri maendeleo katika jamii.
  • Kuratibu na kuhamasisha ushiriki wa jamii katika masuala mtambuka.
  • Kutoa elimu ya haki na wajibu wa jamii na kuwezesha uratibu na usajili wa watoa huduma za msaada wa kisheria katika ngazi ya mikoa na wilaya.
  • Kuelimisha jamii faida za miradi mikubwa ya kitaifa kwa maendeleo ya taifa na fursa kwa jamii.    


      Mafanikio ya Idara

Idara imefanikiwa kufikia ufanisi mkubwa kwenye utekelezaji wa majukumu yake. Mathalani, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kuanzia 2015/2016 hadi 2019/2020, idara imetekeleza majukumu yafuatayo kwa mafanikio makubwa kama ifuatavyo:

  • TASAF awamu ya tatu imefanikiwa kuhawilisha fedha jumla ya shilingi 7,527,190,000/= kwa kaya maskini kutoka kwenye vijiji 94 kati ya vijiji 134. Kwa mwaka 2015/2016 jumla ya kaya maskini 10,476 zilinufaika, mwaka 2016/2017 kaya maskini 10,101 zilinufaika, kaya maskini 9,989 zilinufaika katika kipindi cha mwaka 2017/2018, kaya maskini 9,864 katika mwaka wa 2018/2019 na kaya maskini 9,823 mwaka 2019/2020.
  • Wanufaika wa TASAF awamu ya tatu wameweza kutumia ruzuku wanayopewa kununua chakula, kumudu kuwapeleka watoto wa chini ya miaka mitano kwenye zahanati, vituo vya afya na hospitali kuhudhuria kliniki kwa ajili ya kupatiwa huduma ya afya, kuboresha huduma ya afya kwa kujiunga na mfuko wa bima ya afya ya jamii (CHF) pamoja na kugharamia mahitaji ya elimu kwa watoto wao wanaosoma kwenye shule za msingi na sekondari.
  • Idara imehamasisha uudwaji wa vikundi vya ujasiliamali biashara ambapo jumla ya vikundi 522 vilianzishwa vikihusisha vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.
  • Idara ilitoa mafunzo ya ujasiliamali wa biashara kwa vikundi 184 vyenye jumla ya wanawake 757 na wanaume 163.
  • Idara imeratibu utoaji wa mikopo yenye thamani ya shilingi 323,500,000/= kwa jumla ya vikundi 109 vikiwemo 82 vya wanawake, 21 vya vijana na 6 vya walemavu vyenye jumla ya wanufaika 756 (ambapo wanawake ni 585, vijana ni 135 na walemavu 36). Kati ya fedha hizo, shilingi 245,000,000/= ni mchango wa Halmashauri ya Wilaya kupitia 10% ya mapato ya ndani na kiasi kingine ni fedha za mikopo zilizotolewa na Wizara ya Utamaduni na Vijana pamoja na marejesho ya mikopo ya vikundi (revolving fund).
  • Idara imefanikiwa kutoa elimu ya maendeleo ya jinsia pamoja na kuanzisha kamati za ulinzi wa wanawake na watoto kwenye kata 33 na vijiji 134.
  • Idara imetoa miongozo ya usajili na uratibu kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali (NGOs) yapatayo 18 na kufuatilia shughuli za mashirika haya kama zinazingatia Sera ya mwaka 2001 na Sheria Na.24 ya mwaka 2002 zinazosimamia Mashirika Yasiyo ya Kiserikali pamoja na kanuni na miongozo mbalimbali. Hadi Juni 2020, kuna jumla ya mashirika 6 yenye miradi inayoendelea kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ambayo ni ASANTE AFRICA FOUNDATION, CHAMAVITA, YOUTH PEACE MAKERS, IMPROVING TANZANIA FOUNDATION, ABILIS FOUNDATION na LEVO. Miradi inayotekelezwa na mashirika haya imejikita katika sekta za Elimu, Afya, Maji, Uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, Mazingira, kutokomeza ukatili wa kijinsia na mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI.
  • Idara imetekeleza shughuli za mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI kwenye kata 33 na vijiji 134 kwa kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi na kutokomeza unyanyapaa dhidi ya watu wenye VVU kupitia warsha, mikutano, makongamano na maadhimisho mbalimbali ikiwemo Siku ya UKIMWI Duniani, Siku ya Wanawake Duniani, Siku ya Familia na Siku ya Mtoto wa Afrika.
  • Idara imehamasisha na kuwezesha watu wenye VVU na UKIMWI kuanzisha jumla ya vikundi 32 vya ufugaji wa mbuzi na nyuki kwa ajili ya kuimarisha vipato vya familia zao.
  • Elimu ya kukabiliana na athali za mabadiliko ya tabia nchi kwenye kilimo na  rasilimali za misitu na maji imetolewa kwa jamii kwenye kata 33 za Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto.
  •  Idara imesimamia utekelezaji wa Sheria ya Mtoto Na.21 ya mwaka 2009 na Mpangokazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) kwa kuunda kamati za ulinzi wa wanawake na watoto kwenye kata 33 na vijiji 134 pamoja na kutoa elimu juu ya haki ya mtoto kwenye vijiji na kata.

Changamoto za Idara

Idara inakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazochangia kushindwa kutekeleza shughuli zake kama zilivyopangwa. Changamoto hizo ni kama zifuatazo:

  • Uhaba wa rasilimali fedha umechangia kutofikia ufanisi mkubwa wa utekelezaji wa shughuli za idara.
  • Baadhi ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vilivyopewa mikopo kushindwa kurejesha fedha za mikopo kwa wakati kulingana na mikataba ya makubaliano.
  • Athari za mabadiliko ya tabia nchi kwenye kilimo na rasilimali maji zimeendelea kuongeza umaskini wa kaya kwa kupunguza kipato kitokanacho na kilimo pamoja na wanawake na watoto kutumia masaa mengi kutafuta maji badala ya kuzalisha mali ama kuhudhuria vipindi vya masomo shuleni.
  • Baadhi ya wanajamii wangali wanafuata mila potofu kama kurithi wajane na kutakasa misiba zinazochangia maambukizi mapya ya VVU.
  • Kushamiri kwa migogoro ya familia inayochangia wanawake na watoto kutelekezwa na hivyo kukosa haki zao za msingi pamoja na kunaongeza idadi ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi. Wanawake na watoto wanaotelekezwa hukosa mahitaji muhimu kama chakula, masomo na mavazi pamoja na kuwa hatarini kwa kufanyiwa ukatili wa kijinsia ikiwemo kubakwa.
  • Baadhi ya walengwa wa ruzuku ya TASAF awamu ya tatu kutoka kaya maskini kushindwa kutumia fedha wanazolipwa kugharamia mahitaji ya msingi kama chakula, afya, elimu ama kuanzisha miradi ya kuzalisha kipato. Badala yake huzielekeza fedha hizo kwenye matumizi mengine yasiyo ya msingi kama vile unywaji wa pombe na hivyo kushindwa kufikia lengo la kutokomeza hali ya umaskini wa kaya.

Dira

Idara kuwa kinara katika kutoa huduma kwa uwazi kufikia matokeo ya kijamii na kiuchumi kwa maendeleo endelevu ifikapo 2025.

 

Dhamira

Idara kutoa huduma bora za kiuchumi na kijamii kwa uwazi kwa kutumia vizuri rasilimali zilizopo kuboresha ustawi wa jamii ili kufikia maendeleo endelevu.

Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE MAFUNZO UANDIKISHA WA WAPIGA KURA NA UENDESHAJI MFUMO WA UANDIKISHAJI WA (BVRS) February 08, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA KATA YA MNAZI February 19, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III KUANZIA TAREHE 17/03/2021-18/03/2021. March 08, 2021
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA LUSHOTO ANAWATANGAZIA WANANCHI WOTE KUWA VIKUNDI VYOTE VYA KIJAMII VYA KUWEKA NA KUKOPA (VICOBA, VSLA, HISA, LIMCA NK) April 06, 2021
  • Agalia

Habari mpya

  • MHE. KUBECHA AKABIDHI NG’OMBE BORA WA MBEGU KWA WAFUGAJI WA TARAFA YA UMBA

    August 12, 2024
  • MHE. KUBECHA AKABIDHI NG’OMBE BORA WA MBEGU KWA WAFUGAJI WA TARAFA YA UMBA

    August 12, 2024
  • MKUU WA WILAYA YA LUSHOTO AFANYA ZIARA KATA YA MANOLO

    July 03, 2024
  • MKUU WA WILAYA YA LUSHOTO AFANYA ZIARA KATA YA MANOLO

    July 03, 2024
  • Agalia

Video

HOTUBA FUPI YA KATIBU MWENEZI KITAIFA WA KATI WA ZIARA FUPI ALIYOIFANYA KATIKA WILAYA YA LUSHOTO
Video nyingine

Maunganisho ya haraka

  • organisation structure
  • COUNCIL HISTORY
  • TAMISEMI

Tovuti zenye Mahusiano

  • TOVUTI YA MKOA WA TANGA
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2019
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • National website
  • UTUMISHI

Waangaliaji wa nje

world map hits counter

Waangaliaji wa ndani

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MAGUZONI, 18 BARABARA YA HALMASHAURI, 21782 Lushoto,Tanga

    Postal Address: P.O.BOX 32 Lushoto

    Telephone: +255(027)2977216

    Mobile: +255 755 723 374

    Email: ded@lushotodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto.Haki zote zimeifadhiwa