• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Lushoto District Council
Lushoto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto

  • mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Historia
    • Dira na Dhamira
      • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
      • Muundo
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Utumishi na Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufatiliaji
        • Planning
      • Afya
        • Healthy
      • Fedha na Biashara
        • Finance
      • Elimu ya Msingi
        • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya sekondari
        • Elimu ya sekondari
      • Maji
        • water sector
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
        • Agriculture and Irrigation
      • Huduma za ufugaji
        • Huduma za ufugaji
      • Maliasili Ardhi na Mipango Mji
      • Maendeleo ya Jamii Wanawake Vijana Watoto na Wazee
        • Community development
      • Ujenzi na Zima Moto
        • Works and fire rescure
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
        • Internal Auditor unit
      • Teknolojia ya Habari na mawasiliano
        • Information communication and public Relation
      • Manunuzi na Ugavi
        • Manunuzi na Ugavi
      • Mazingira na Usafi
        • Environment and sanitation
      • Uchaguzi
        • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezajia
    • Vivutio vya Utalii
      • Tourist attraction investiment area
    • Kilimo
      • Agriculture Investment Areas
    • Mazao ya misitu
      • Forest products
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
      • Health services offered
    • Huduma za Elimu
      • Education services offered
    • Huduma za Kilimo
      • Agriculture services offered
    • livestock and fisheries services
      • livestock and fisheries services offered
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Uchumi Uongozi na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati za maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba mbalimbali
    • Ghala la Picha

NAIBU WAZIRI WA MAJI AHAIDI KUMALIZA TATIZO LA MAJI TARAFA YA MTAE

Imetumwa: January 9th, 2024

NAIBU Waziri wa Maji, Eng. Maryprisca Mahundi (Mb), ameahidi kumaliza tatizo la maji kwenye Tarafa ya Mtae, iliyopo katika Jimbo la Mlalo, Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto, wilayani Lushoto, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa lengo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan la kumtua mama ndoo kichwani.

Akizungumza na wananchi kwenye mikutano ya hadhara katika Kata ya Mbaru na Rangwi, Eng. Mahundi, alisema kwamba Wizara yake chini ya Waziri wa Maji, Mhe. Juma Awesso ina taarifa juu ya changamoto za maji zinazoikabili Tarafa ya Mtae hii ni kutokana na swali ambalo aliwahi kuulizwa bungeni na Mbunge wa Jimbo la Mlalo, Mhe. Rashid Shangazi.

Hivyo, aliwataka wananchi kuendelea kuwa na subra na kuwa na imani na serikali yao kwa sababu, walipotoka ni mbali kuliko wanapokwenda na kueleza kuwa kwa sasa watakuwa na mipango ya aina mbili kwenye kutatua tatizo la maji kwenye Tarafa ya Mtae, hususani Kata za Mbaru, Rangwi na Sunga.

Alisema kwamba kwa kuanzia wanaenda kuboresha mradi mkongwe wa ENGOMAKA ili uweze kufanya kazi, huku serikali ikienda kutafuta suluhisho la muda mrefu, ambapo kwa sasa kuna Msanifu Mshauri ambaye anafanya kazi ya kutafuta vyanzo vikubwa zaidi vya maji kwenye maeneo hayo ili waweze kutengeneza mradi mkubwa zaidi kwenye mwaka ujao wa fedha.

Eng. Mahundi ametoa maagizo kwa RUWASA Wilaya ya Lushoto, kuhakikisha hadi kufikia mwisho wa mwezi wa pili, wanakuwa tayari wametatua matatizo ya mradi wa ENGOMAKA, ili wananchi wapate maji kwa kipindi hiki wakati serikali ikienda kutafuta suluhisho la muda mrefu kwenye mwaka ujao wa fedha.

Aliongeza kusema kwamba serikali itamlipa shilingi milioni 100, Msanifu Mshauri kwa ajili ya kutafuta chanzo cha uhakika na kuutaka uongozi wa Bonde la Pangani kushirikiana na mtaalamu huyo ili kufanikisha upatikanaji wa chanzo cha uhakika ili kumaliza kabisa tatizo la maji Tarafa ya Mtae.

Lakini, Eng. Mahundi aliendelea kusema kwamba ikiwa kitakosekana chanzo cha uhakika basi, serikali italazimika kuchimba visima virefu lengo likiwa ni kumaliza kabisa changamoto ya maji Tarafa ya Mtae na kumtua Mama ndoo kichwani kwa vitendo.

Katika hatua nyingine; Wananchi wa Kata ya Lukozi, waliotanda barabarani walifanikiwa kusimamisha msafara wa Eng. Mahundi na kumuwasilishia kero yao ya maji, ambapo aliwaahidi kutatua changamoto hiyo huku akiwasihi kuendelea kutunza vyanzo vya maji.


Matangazo ya Kawaida

  • KUITWA KWENYE MAFUNZO UANDIKISHA WA WAPIGA KURA NA UENDESHAJI MFUMO WA UANDIKISHAJI WA (BVRS) February 08, 2025
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA KATA YA MNAZI February 19, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA III KUANZIA TAREHE 17/03/2021-18/03/2021. March 08, 2021
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA LUSHOTO ANAWATANGAZIA WANANCHI WOTE KUWA VIKUNDI VYOTE VYA KIJAMII VYA KUWEKA NA KUKOPA (VICOBA, VSLA, HISA, LIMCA NK) April 06, 2021
  • Agalia

Habari mpya

  • MHE. KUBECHA AKABIDHI NG’OMBE BORA WA MBEGU KWA WAFUGAJI WA TARAFA YA UMBA

    August 12, 2024
  • MHE. KUBECHA AKABIDHI NG’OMBE BORA WA MBEGU KWA WAFUGAJI WA TARAFA YA UMBA

    August 12, 2024
  • MKUU WA WILAYA YA LUSHOTO AFANYA ZIARA KATA YA MANOLO

    July 03, 2024
  • MKUU WA WILAYA YA LUSHOTO AFANYA ZIARA KATA YA MANOLO

    July 03, 2024
  • Agalia

Video

HOTUBA FUPI YA KATIBU MWENEZI KITAIFA WA KATI WA ZIARA FUPI ALIYOIFANYA KATIKA WILAYA YA LUSHOTO
Video nyingine

Maunganisho ya haraka

  • organisation structure
  • COUNCIL HISTORY
  • TAMISEMI

Tovuti zenye Mahusiano

  • TOVUTI YA MKOA WA TANGA
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2019
  • TOVUTI YA TAMISEMI
  • National website
  • UTUMISHI

Waangaliaji wa nje

world map hits counter

Waangaliaji wa ndani

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    MAGUZONI, 18 BARABARA YA HALMASHAURI, 21782 Lushoto,Tanga

    Postal Address: P.O.BOX 32 Lushoto

    Telephone: +255(027)2977216

    Mobile: +255 755 723 374

    Email: ded@lushotodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki©2018 Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto.Haki zote zimeifadhiwa